Showing posts with label Home. Show all posts
Showing posts with label Home. Show all posts

Saturday, May 2, 2015

KIVUMBI CHA POLISI NA MWENDESHA BODABODA MLIMANI CITY

BODABODA mmoja ambaye jina lake halikufahamika mara moja, mwanzoni mwa wiki hii alionja joto ya jiwe baada ya kuhenyeshwa na polisi kufuatia kitendo chake cha kukataa kutii sheria bila shuruti, alipotaka kusababisha ajali Barabara ya Chuo Kikuu, eneo la Mlimani City, jijini Dar.
 Dereva bodaboda akidhibitiwa na polisi.

Shuhuda wa sakata hilo aliliambia gazeti hili kuwa, mwendesha bodaboda huyo aliyekuwa akitokea Mwenge kuelekea Chuo Kikuu, alisimama barabarani ili kuzungumza na abiria aliyemsimamisha ndipo askari wa Jeshi la Polisi wanaotembea na pikipiki, walimfuata na kuzungumza naye.
 Dereva bodaboda akipambana na polisi.

 “Polisi walimuuliza kwa nini amesimama barabarani kwani kitendo hicho kingeweza kusababisha ajali, walimtaka awape funguo kwa kile walichosema kitendo hicho ni ukiukwaji wa sheria, lakini bodaboda alikuja juu na kuanza kutaka kupambana na polisi,” alisema shuhuda huyo.
Inadaiwa kuwa baada ya polisi hao waliokuwa na silaha zao za moto, kuzozana kwa muda bila mafanikio na bodaboda huyo, walinzi wanaolinda lango la kuingilia Mlimani City waliungana na polisi kumtaka mwendesha pikipiki huyo kukubali kufuata sheria.

 Wakimtia nguvuni.

 “Baada ya kuona askari wa pikipiki na walinzi wamemzunguka mwenzao, bodaboda mwingine naye alisogea na pikipiki yake pale ili aweze kumsaidia, lakini naye akajikuta akiibwaga pasipo kufanikiwa kumnasua dereva huyo ambaye alikuwa jeuri,” alisema shuhuda mwingine.Askari hao walifanikiwa kumtaiti mwendesha bodaboda huyo na kwenda naye kituoni kwa maelezo zaidi.

SHOO YA ZARI ALL WHITE PARTY YAFUNIKA JIJINI DAR

 Diamond akiwachengua mashabiki kwa wimbo wake wa Nasema Nawe aliomshirikisha Malkia wa Taarab, Khadija Kopa.
 Malkia wa Taarab nchini, Khadija Kopa akiimba sambamba na Diamond Wimbo wa Nasema Nawe.

 Mwanamuziki wa Bongo Fleva, Shetta akiwarusha mashabiki waliofika katika Usiku wa Zari All White Party.
 Diamond na Nay wa Mitego wakiimba ngoma yao ya Muziki Gani.
 Mashabiki wakijiachia.

 Diamond Platnumz akizikonga nyoyo za mashabiki.
 Ray Kigosi na Mama Rolaa nao ndani.
 Diamond akicheza na mashabiki wake.
Nyomi iliyohudhuria shoo hiyo.

ALI KIBA AVAMIWA USIKU WA KUAMKIA LEO

 Msanii wa Bongo Fleva, Ali Kiba

 MSANII wa Bongo Fleva, Ali Kiba usiku wa kuamkia leo akiwa nyumbani kwake Kunduchi jijini Dar es Salaam, alivamiwa na kundi la watu wapatao 20 wanaodhaniwa kuwa ni majambazi.

 Ali Kiba akiwa katika pozi.
 Watu hao waliokuwa na silaha za aina tofauti yakiwemo mapanga, visu na silaha za moto walifanikiwa kuvunja kuingia ndani na kuwadhuru baadhi ya ndugu wa Ali Kiba na kuiba mali na kila kitu ambacho waliweza kubeba, walimpiga na kumtesa mlinzi wa nyumba hiyo wakimtaka awaonyeshe alipo Ali Kiba, hata hivyo hawakufanikiwa kumpata na wakaondoka muda mfupi kabla ya polisi hawajafika nyumbani kwa staa huyo baada ya kupigiwa simu na majirani.
Ikiwa utakuwa na taarifa zozote zitakazosaidia kupatikana kwa majambazi hao, unaweza kutoa taarifa katika kituo cha polisi ulicho karibu nacho.

Global

Wednesday, April 29, 2015

MUNGU MKUBWA: TAZAMA PICHA JINSI KICHANGA HIKI KILIVYOOKOLEWA KWENYE KIFUSII HUKO NEPAL

Mtoto mwenye umri wa miezi minne ameokolewa kwenye kifusi cha jengo llililoanguka kufuatia tetemeko kubwa la ardhi huko Nepal.



MIILI YA WAUZA MADAWA YA KULEVYA WALIOUAWA INDONESIA YAANZA KURUDISHWA MAKWAO.

Ndugu wa marehemu waliouawa baadaya kukutwa na hatia yakuingiza madawa ya kulevya nchini Indonesia wakiwa ndani ya gari la wagonjwa liliobeba mwili ya ndugu yao mara baada ya kuupokea toka gerezani katika kisiwa cha Nusa Kambangan.

INDONESIA YAJITETEA KWA KUUA WAUZA UNGA 8, YASEMA HIYO NI VITA DHIDI YA DAWA ZA KULEVYA.

Waustralia wawili waliouawa

 Indonesia imetetea uamuzi wake wenye utata wa kuamua kuwauwa walanguzi wanane wa dawa za kulevya wakiwemo raia saba wa kigeni, ikisema kuwa hivyo ni vita dhidi ya biashara ya mihadarati.

Kwa upande wake, Australia imemuita nyumbani balozi wake Nchini Indonesia, kama hatua ya kulalamikia kuuwawa kwa raia wake wawili waliohusika na ulanguzi huo.
Waziri mkuu Tony Abbott, anasema kuwa hata ingawa anaheshimu utawala wa Indonesia kama taifa huru, uhusiano wa mataifa hayo mawili hautaendelea kama kawaida kufuatia mauwaji ya wa-australia hao wawili.
Mkuu wa sheria Nchini Indonesia, Muhammad Prasetyo, ameelezea hatua hiyo ya Ausralia kama hasira za muda mfupi tu.
 Moja ya majeneza ya wale waliouawa


Waustralia hao wawili waliuwawa kwa kupigwa risasi na kikosi maalum cha wauwaji kwa pamoja na washukiwa wengine sita wa ulanguzi wa mihadarati, watano kati yao walikuwa raia wa kigeni.
Licha ya vilio vya kuwasamehe watu hao kutoka kwa mataifa ya dunia, Indonesia iliamua kwa vyovyote kuwauwa.
Kuuwawa kwa mfungwa wa tisa, raia wa Ufilipino, Mary Jane Veloso, kumecheleweshwa na Rais Joko Widodo, baada ya mwanamke mmoja kujiwasilisha kwa polisi nchini Ufilipino, akisema kuwa ndiye aliyemhadaa mfungwa huyo mwanamke mwenzake, kupeleka dawa za kulevya hadi Indonesia.
Brazil nayo inasema kuwa kuuwawa kwa raia wa pili wa Brazil Nchini Indonesia, katika kipindi cha miezi minne, ni hatua ya kutamausha na ambayo tayari imeyumbisha vibaya uhusiano wa kidiplomasia wa mataifa hayo mawili.

BBC

ESCROW YAMPAISHA KAFULILA, APATA TUZO YA UTETEZI WA HAKI.

Mbunge wa Kigoma Kusini (NCCR Mageuzi), David Kafulila akikabidhiwa Tuzo ya utetezi wa haki za binadamu ya mwaka 2014, Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora Tom Nyanduga, Dar es Salaam jana.  Kulia ni Mwenyekiti wa Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu nchini, Martina Kabisama.  


Dar es Salaam. Sakata la uchotwaji wa fedha katika Akaunti ya Tegeta Escrow limemng’arisha Mbunge wa Kigoma Kusini (NCCR- Mageuzi),  David Kafulila baada ya kutunukiwa tuzo ya kutambua mchango wake katika kufichua ufisadi huo uliohusisha uchotwaji wa Sh306 bilioni kutoka Benki Kuu ya Tanzania (BoT).
Katika sakata hilo, mawaziri wawili walipoteza nyadhifa zao pamoja na Mwanasheria Mkuu wa Serikali baada ya Ripoti ya Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali kuwahusisha na sakata hilo. Maofisa wengine kadhaa wa Serikali wamesimashwa au kufunguliwa mashtaka kutokana na kuhusika kwao kwenye ufisadi huo.
Sakata hilo lililoteka kwa kiasi kikubwa mkutano wa Bunge wa 16 na 17 kabla ya kufika bungeni,  liliibuliwa na Gazeti la The Citizen, linalochapishwa na Kampuni ya Mwananchi Communications Ltd na Kafulila kuwasilisha hoja ndani ya Bunge ili kujadiliwa.
Tuzo aliyopewa Kafulila jana na Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu unaounganisha asasi za kiraia zinazotetea haki za binadamu (THIRD-Coalition), ni moja kati ya tuzo tatu zilizotolewa kwa Watanzania walioonyesha ujasiri katika kutetea haki za binadamu nchini.
Wengine ni Maanda Ngoifiko wa asasi ya kiraia, inayotetea haki za binadamu ya PWC kutoka  Loliondo  wilayani Ngorongoro, na Mwandishi wa Gazeti la Mwananchi, Salma Said aliyetishiwa kuuawa baada ya kuonyesha msimamo wa kukataa shinikizo la kukubaliana na muundo wa Muungano wa serikali mbili wakati wa Bunge Maalumu la Katiba.
Kwa mujibu wa THIRD-Coalition, vigezo vilivyotumika kuwapata washindi hao vilizingatia mazingira ya kazi na hali hatarishi aliyokutana nayo mshindi wa tuzo hiyo, ikiwamo taarifa zilizokusanywa kupitia ripoti za matukio ya ukiukwaji wa haki za binadamu kwa mwaka jana.
Baada ya kukabidhiwa, Kafulila alisema tuzo hiyo ni mwanzo wa hatua nyingine ya kuendelea kuibua ufisadi ndani ya Serikali.
“Nimepata ujasiri na kuamini kwamba siko peke yangu katika vita hii, nashukuru kupata tuzo hii, lakini nashukuru zaidi ushirikiano nilioupata kwa mhariri wa gazeti la The Citizen, ambaye alinipatia nyaraka nne za kuanzia,” alisema Kafulila.
“Hata hivyo, ninasikitishwa kuona bado Tanesco wakiendelea kulipia Dola 4 bilioni za capacity charge kwa kampuni hiyo ya ITPL, wakati hukumu iliyotolewa na Mahakama ya ICSID ya Uingereza Februari 12, mwaka jana inasema haikuwa sahihi tozo hiyo, lakini bado kiwango hicho kinaendelea kulipiwa.”
Salma alisema pamoja na vitisho ambavyo bado ameendelea kukutana navyo mpaka sasa kutoka kwa baadhi ya wabunge wa lililokuwa Bunge la Katiba, bado msimamo wake utaendelea kuwa palepale.
Aidha, alisema vita iliyopo kwa sasa imehamia kwenye harakati za Baraza la Katiba la Zanzibar ambalo linaendesha elimu kwa Wazanzibari kuhusu Katiba Inayopendekezwa. “Mimi ni mjumbe wa Baraza hilo na kwa sasa hawapendi kuona tukielimisha ukweli wa Katiba hiyo na badala yake wanataka kueleza mazuri tu. Hilo tumesema haliwezekani.”

 Miswada ya sheria

Katika hatua nyingine, Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB), Tom Nyanduga aliyekabidhi tuzo hizo, amewataka wadau wote wa haki za binadamu nchini kufungua kesi mahakamani kupinga miswada hiyo itakayosainiwa na Rais wakati wowote kuanzia sasa.
Nyanduga aliwataka kutoendelea kulalamika tu na badala yake wachukue hatua hiyo ili kujihakikishia haki imetenda kwani Mahakama ndiyo sehemu itakayopima uhalali wa sheria hizo kama zinawapokonya uhuru na haki zao kikatiba. Miswada hiyo ni ule wa Sheria ya Takwimu ya mwaka 2015 na Sheria ya Makosa ya Mitandao ya mwaka 2015.
Kauli hiyo inajibu madai ya Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), kupitia viongozi wake, ambao juzi walisema ikiwa Rais Jakaya Kikwete atasaini miswada hiyo kuwa sheria, watakwenda mahakamani kupinga hatua hiyo licha ya Ikulu kueleza msimamo ikisisitiza kusainiwa miswada hiyo.
Akizungumza jana wakati wa kusherehekea Siku ya Watetezi wa Haki za Binadamu nchini, jijini hapa, Nyanduga alisema: “Wasilalamike tu kuna utaratibu ambao wanaweza kufikisha madai yao mahakamani bila kujali kama rais atasaini au la kwani yeye (Rais) anayo mamlaka yake kikatiba,ila wakienda mahakamani haki itatendeka kama kuna ukandamizaji umefanyika,” alisema Nyanduga.
Mbali na utoaji wa tuzo hizo, umoja huo pia ulizindua ripoti ya taarifa ya hali ya upiganiaji wa haki za binadamu kwa mwaka 2014, ambayo inaonyesha kuwa kesi tano zilifikishwa mahakamani, kesi 20 zilizoripotiwa na waandishi mbalimbali wa habari nchni, wakidai kufanyiwa vitisho huku ikielezea maombi ya uboreshaji wa sheria 29 kandamizi katika uhuru na haki za wananchi kupata taarifa.
Mwenyekiti wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Dk Hellen Kijo Bisimba alikuwa miongoni mwa wadau wa umoja huo ambaye alisema kundi la wanaokandamiza haki isitendeke nchini linazidi kujitokeza, huku likijenga hofu kwa watetezi wa haki.
“Kundi hilo halipendi kukosolewa na hata likiona kuna utetezi sehemu fulani, basi yule anayetetea atakuwa kwenye wakati mgumu. Mfano kuna vipingamizi vya kuzuiwa na wakuu wa wilaya, wakuu wa mikoa ili tusitoe elimu juu ya Katiba inayopendekezwa katika baadhi ya wilaya nchini. Hatuwezi kukubaliana na hali hiyo lazima tuone haki ikitendeka kwa wote,” alisema Dk Hellen.

MWANANCHI

Jeshi la Nigeria lawaokoa mabinti 293

Jeshi nchini Nigeria 

 Jeshi la Nigeria limesema limewaokoa watoto wa kike mia mbili na tisini na tatu kutoka katika kambi ya Boko Haram iliyoko katika msitu wa Sambisa, kaskazini mashariki mwa nchi hiyo. Jeshi hilo limesema watoto hao waliokolewa si kati ya wale waliotekwa mwaka mmoja uliopita na kundi la kiislamu katika eneo la Chibok.
Jeshi limeiambia BBC kwamba wanawake na watoto hao wa kike walikutwa katika kambi nne tofauti ambapo silaha pia zimekamatwa,Msemaji wa jeshi amesema waliwapata wasichana hao baada ya kuziharibu kambi hizo.
"ni muda mfupi tu uliopita, wanajeshi wetu wameingia katika msitu wa Sambisa, kutokea upande wa Alafa, ambapo walikuta kambi nne zinazomilikiwa na wapiganaji na kuziharibu, hapo ndipo walipogundua kuwa kuna wasichana wapatao mia mbili na wanawake tisini na tatu."
Kwa sasa jeshi limezuiwa kutoa utambulisho wa wasichana hao. Hata hivyo, jeshi limethibitisha kwamba wasichana hao sio wale wanafunzi waliotekwa katika mji wa Chibok.
"tuko katika mchakato wa kuwachunguza hawa wasichana ili tuweze kubaini utambulisho wao, lakini kitu kimoja nataka nikiweke wazi kwa umma, tunapotaja idadi ya wasichana mia mbili, tayari watu wanaanza kufikiria wasichana mia mbili wa Chibok waliotekwa mwaka jana, hawa sio wasichana wa Chibok, tutaendelea kuwajuza kadri muda unavyokwenda iwapo kutakuwa na taarifa zozote. "

BBC

Tuesday, April 28, 2015

Mgodi wa Tanzanite One wamwaga ajira 1,280

 Waziri wa Nishati na Madini, George Simbachawene (kulia) akipata maelezo kwa wakurugenzi wa kampuni ya Tanzanite One, Faisal Juma Shabhai na Hussein Gonga


Arusha, Kampuni ya Tanzanite One ambayo sasa inamilikiwa na wazawa, imeongeza ajira kwa vijana kutoka 700 hadi 1,280 ili kukabiliana na tatizo hilo nchini.
Wakizungumza na waandishi wa habari katika maonyesho ya madini ya vito yanayoendelea jijini hapa, wakurugenzi wa Kampuni ya Sky Associate Ltd iliyonunua asilimia 50 ya hisa ndani ya Tanzanite one, Hussein Gonga na Faisal Juma walisema wameanzisha pia mafunzo ya kukata kna usanifu wa madini.
Gonga alisema Sky Associate na Shirika linaloshughulikia Madini Tanzania (Stamico) ambao ndiyo wamiliki wa Tanzanite One, wameongeza maeneo ya uchimbaji madini ili kuhakikisha wanaongeza ajira kwa vijana wengi wanaotafuta ajira za uchimbaji katika migodi ya madini.
Alisema katika mafunzo ya ukataji na usanifu wa madini, vijana hufundishwa jinsi ya kuyaongezea thamani na wanaohitimu hupatiwa mashine.
Awali, Mkurugenzi mwenza wa Tanzanite One, Faisal Juma alisema mipango ya kuongeza ajira na kutoa mafunzo ya usanifu wa madini itasaidia kuboresha sekta ya madini nchini.
Juma alisema Tanzanite One kama kampuni kubwa nchini ya uchimbaji wa madini ya vito, itahakikisha inashirikiana na Serikali na wadau wengine kufanya mapinduzi katika sekta ya madini ili Watanzania wengi waweze kunufaika.
Kamishna wa Madini Tanzania, Paul Masanja akizungumza katika maonyesho hayo, aliwataka wamiliki wa migodi na wachimbaji kushirikiana kuboresha sekta ya madini kwa kuhakikisha hawauzi wa kuyatorosha nje ya nchi madini ghafi.
Alisema Serikali itaendelea kushirikiana na wadau wa madini kuhakikisha wanapata masoko ya madini yao na alipongeza jitihada za kuwapa mafunzo vijana juu ya ukataji wa madini.

REVEALED: $350 million (675 BILLION SHILLINGS) stolen from Tanzanians in Vodacom scandal





• Tycoons Tanil Somaiya & Rostam Aziz implicated in the scam
• Vodacom Tanzania MD Rene Meza receives $5 million bribe to keep silent
• Tax worth over 121.5 billion/- evaded in the deal
• PCCB, TCRA, TRA caught napping in massive fraud bigger than EPA and Escrow combined
A staggering $350 million (over 675 billion shillings) was stolen from Tanzanians in a massive scandal involving the sale of pirated electronic recharge vouchers from Vodacom Tanzania to customers.
The scam, which is bigger than the Bank of Tanzania’s infamous external payment arrears (EPA) and IPTL Tegeta escrow account scandals combined, involves Tanil Somaiya, a business tycoon behind several dubious deals in Tanzania, including the military radar transaction with Britain’s BAE Systems.
The production of the electronic recharge vouchers followed the signing of a contract between Vodacom Tanzania and Tanil’s Shivacom Group in 2007/08. This means that Shivacom acted both as a Vodacom super dealer and printer and supplier of electronic recharge vouchers, an obvious conflict of interest.
In the elaborate scandal, Tanil’s company, Shivacom Group, printed millions of pirated 500 shillings electronic recharge vouchers (Jero Jero) between 2008 and 2012 and colluded with other companies owned by Fred Lowassa (Alphatel) and TIB Development Bank Managing Director Peter Noni (Planetel) to distribute the vouchers across Tanzania.
Fred Lowassa is the director of Alphatel, a Vodacom super dealer, while Noni, a former senior Bank of Tanzania (BoT) official, also owns another Vodacom super dealer, Planetel.
Together, Shivacom colluded with Alphatel and Planetel to carry out the massive fraud involving the production, distribution and sale of pirate electronic recharge vouchers worth over 675 billion shillings without Vodacom’s knowledge until the scam was unearthed in 2012.
There was also rampant tax evasion in the scandal with Value Added Tax (VAT) worth more than 121 billion shillings evaded by Shivacom and its conspirators, which is a serious criminal offence.
Senior officials at Tanzania government regulatory and watchdog agencies such as the Tanzania Revenue Authority (TRA), the Tanzania Communications Regulatory Authority (TCRA) and the Prevention and Combating of Corruption Bureau (PCCB) were either complicit in the scandal or were caught napping.
Shivacom alone distributed more than half of the fake recharge vouchers, while the other pirate vouchers were distributed by its conspirators — Alphatel and Planetel.
The “Jero Jero” vouchers are the most fast-moving electronic recharge vouchers in Tanzania, with Shivacom printing hundreds of millions of fake vouchers using pins provided by Vodacom Tanzania.
The scandal not only caused Vodacom Tanzania huge financial loss, it also resulted in the detrimental loss of customer confidence. This is partly attributed to Vodacom Tanzania losing its dominance in Tanzania’s mobile phone industry, with Airtel and Tigo now threatening to wrestle away the company’s market share.
Insiders say Vodacom Tanzania’s MD, Rene Meza, found out about the scandal after just arriving in Tanzania from Kenya to take up the position of Vodacom Tanzania managing director.
“Rene Meza confronted Tanil about the scandal and demanded a $10 million kickback to keep quiet. Tanil arrogantly told him to piss off, so Rene retaliated by instructing Vodacom’s legal counsel to write a letter to Shivacom to terminate the electronic recharge voucher agreement for breach of contract,” said a well-placed source.
“Tanil went to Vodacom South Africa’s Group CEO, Shameel, and gave him a bribe of $400,000. Shameel then instructed Vodacom Tanzania to settle the matter with Shivacom. Rene Meza finally settled for a $5 million bribe from Tanil and Vodacom paid Tanil hefty compensation for termination of the contract despite the obvious fraud.”
Vodacom Tanzania’s lawyers gave legal advice that the contract should be terminated and Shivacom should pay compensation to Vodacom for the fraud. However, after bribes exchanged hands, Shivacom ended being paid a hefty compensation by Vodacom despite perpetrating the massive fraud.
In all this scandal, Tanil used a Dar es Salaam-based lawyer, Dilip Kesaria, to respond to legal queries from Vodacom.
Kesaria, who was disbarred in the United Kingdom for malpractices but fraudulently allowed to operate as a lawyer in Tanzania, is the Principal at Kesaria & Company advocates.
The following is a chronology of key events in the massive 675 billion shillings fraud involving Vodacom Tanzania’s Jero Jero electronic recharge vouchers:
Key Facts and Figures
• 2008. A 10-year agreement comes into effect for Shivacom Tanzania Limited to provide electronic recharge vouchers (EVD) to Vodacom Tanzania Limited. This means that Shivacom effectively played a dual role of being a Vodacom super dealer and EVD supplier in separate agreements.
• 2008-2012. The massive fraud committed by Shivacom over the 5-year period is worth more than $350 million (675 billion Tanzanian shillings), which is bigger than the Bank of Tanzania EPA and Tegeta Escrow account scandals combined. This fraud was done by Shivacom printing TZS 500 electronic recharge vouchers (Jero Jero) fraudulently and distributing them into the market without Vodacom’s knowledge.
Other Vodacom super dealers, including Alphatel and Planetel are also implicated in directly colluding with Shivacom to distribute pirate recharge vouchers.
• 31 July 2012. Vodacom Tanzania Ltd’s Chief Legal & Regulatory Officer writes a letter to Shivacom Tanzania Ltd to formally notify the company about breach of contract. This comes after Vodacom Tanzania Ltd discovered that Shivacom has been engaged in massive fraud over the past 5 years (2008-2012) by printing and distributing pirate electronic recharge vouchers using pin numbers provided by Vodacom. This letter effectively terminated the EVD contract between Vodacom Tanzania Ltd and Shivacom Ltd.
• 3 August 2012. Shivacom responds to Vodacom’s letter, disputing the decision to terminate the EVD contract under advice from Kesaria.
• 3 September 2012. Shivacom Group’s Managing Director, Tanil Somaiya, writes a letter to Vodacom’s Group CEO in South Africa, Shameel Aziz Joosub, requesting a meeting to discuss the EVD contract termination. Tanil succeeds in meeting with Shameeel, who is compromised and orders Vodacom Tanzania to settle the matter with Shivacom and pay compensation to the company for contract termination despite the fraud. The meeting between Tanil and Shameel with other senior Vodacom officials took place on 1 November 2012.
Vodacom Tanzania MD, Rene Meza, receives a bribe of $5 million from Tanil Somaiya to resolve the matter.
• 9 November 2012. Tanil writes a letter to Shameel, saying he was offering his Shivacom Superdealership subscriber base for sale. Shivacom gave Vodacom the right of first refusal and asked for consent to scout around for alternative buyers if Vodacom was not interested in buying the dealership.
• 14 November 2012. Vodacom Tanzania Ltd’s Chief Legal & Regulatory Officer writes a letter to Shivacom offering compensation payment for termination of the contract. This is despite the fact that Vodacom’s lawyers gave legal advice to the firm to terminate the contract with Shivacom given the fact that Shivacom have breached the contract by duplicating TZS 500 vouchers.
• 29 November 2012. Tanil writes a letter to Shameel rejecting Vodacom’s “paltry” compensation offer. Tanil demands hefty compensation for loss of profit, cost of hardware and software of the voucher production equipment and cost of unutilized stock of raw materials.
• 2012-2015. Vodacom settles with Shivacom by paying the company a multi-million U.S. dollar compensation despite the company committing the massive fraud.
To be continued…

HELKOPTA YA NDESAMBURO YAZUA KIZAAZAA MOSHI.

Helikopta iliyotumiwa na Kada wa CCM Buni Ramolle, ikitua katika Uwanja wa Pasua mjini Moshi, Aprili 18 mwaka huu.


Moshi. Helkopta ya Mbunge wa Moshi Mjini, Philemon Ndesamburo, imeleta kizaazaa, baada ya Kada wa CCM, Buni Ramolle ambaye aliikodi kwa ajili ya mikutano yake ya kutangaza nia ya kugombea ubunge katika jimbo hilo, kudai kuwa ni mbovu na ilitaka kumuua.
Kada huyo akaenda mbali na kueleza kuwa kutokana na hitilafu hiyo, ameitaka kampuni ya General Aviation Services (T) Ltd, iliyomkodishia helkopta hiyo, kumrejeshea fedha zake zote alizoilipa kwa ajili ya kuitumia wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba mwaka huu.
Hata hivyo, Ndesamburo ambaye ni mmiliki wa helkopta hiyo kupitia kampuni yake ya Keys Aviation, alikanusha madai hayo akisema kuwa hayana msingi.
“Anasema helikopta ni mbovu wakati ilimpeleka na kumrudisha? Alihoji Ndesamburo na kusisitiza kuwa “tutawaomba wakaguzi wa ndege waifanyie ukaguzi na ripoti hiyo ndio tutaitumia kumshitaki nayo.”
Kuhusu madai ya Ramolle kuwa amerejeshewa fedha zake alizolipa, Ndesamburo alihoji “Tunamrudishia fedha gani wakati hakulipa? Kuwa na Proforma Invoice ndio kulipia?”
Awali taarifa zilieleza kuwa Ramolle alitoa tuhuma hizo, baada ya viongozi wa CCM, kumbana wakimtaka aeleze kwa nini ameamua kutumia helkopta ya Ndesamburo ambaye ni mpinzani wake kisiasa.
Jana Ramolle alitumia mkutano wake na waandishi wa habari kukanusha kuwa helkopta aliyoitumia Aprili 18 mwaka huu ni ya Ndesamburo. Alidai katika mkutano huo kuwa helkopta hiyo aliikodisha kama mteja kutoka kampuni ya General Aviation Services na hajui kama ni ya Ndesamburo.
Lakini tayari Ndesamburo mwenyewe ameshajitokeza hadharani na kudai kuwa helkopta hiyo ni mali yake na kwamba ameingia mkataba wa kuikodisha kwa kampuni ya General Aviation Services (T) Ltd.
Huu ni mchezo mchafu
Kwa mujibu wa Ramolle, kinachofanyika sasa ni mbinu za kumchafua ndani ya chama ili asiaminike na aenguliwe kama alivyoenguliwa mwaka 2010.
Ramolle alisema kutokana na Ndesamburo kudai helkopta hiyo ni yake, tayari kampuni ya General Aviation Services wamemrudishia fedha zake alizokuwa amekodishia na ameishtaki kampuni hiyo kwa Meneja wa TRA mkoa wa Kilimanjaro kutokana na kutompa risiti ya malipo aliyoyafanya. Buni alisema atapambana na waandishi wanaotaka kumchafua kwa kuwa ana mahasimu ndani na nje ya chama na kutaka asiharibiwe kazi yake na siasa.
“Nimechoka kunyanyaswa nimepata madhara makubwa kwa sababu ya siasa nina maadui ndani na nje ya chama nitapambana na yeyote atakayenizushia maneno na mtu asinifuatefuate” alisema.

Chopa siyo maendeleo
Akizungumzia kutumia chopa kwenye mikutano, Ramolle alisema nia ni kuleta ushawishi kwa wananchi ili wahudhurie mikutano na kwamba hekopta si maendeleo.
“Nimechukua (chopa) makusudi ili kuwaonyesha wananchi Chopa si maendeleo, watu wa Moshi wanafikiri chopa ni maendeleo chopa kazi yake ni kuvuta watu na nimeshaiagiza itakuja hii niliyokodisha awali ni mbovu kwanza ingeweza kuniua ile,” alisema.
“Nilitaka watu wajue chopa siyo maendeleo, Ndesamburo alikuwa akiitumia kuwavuta tu. Maendeleo ni uwajibikaji”
Ramolle alisema kwa maslahi ya watu wa Moshi yupo tayari kuchukua uamuzi mgumu iwapo chama kitaengua jina lake . “Nikishinda halafu jina langu likakatwa patachimbika.”

Monday, April 27, 2015

UKISTAAJABU YA MUSA....... HUWEZI AMINI BABAKE KIM KARDASHIAN SASA NI MWANAMKE!!!!

Babake Kim Kardashian

Bruce Jenner aliyekuwa mwariadha bora duaniani kabla ya kuwa nyota wa kipindi cha televisheni na familia moja maarufu duniani ''The Kardashians''. sasa amefichua siri ambayo amekuwa akiificha kwa miaka mingi.
''Kwa nia na madhumuni yote, mimi ni mwanamke.'' Jenner aliambia Sawyer kutoka ABC katika mahojiano maalum yaliopeperushwa hewani siku ya Ijumaa.
''Watu wananiona tofauti,wananiona kama mwanaume, lakini moyo na roho yangu na kila kitu ninachofanya maishani ni sehemu yangu.'' Jenner ambaye ana umri wa miaka 65 amesema. '' Upande huu wa kike ni sehemu yangu.
hivi ndivyo mimi nilivyo.''
 
Katika masaa ya mahojiano na Diane Sawyer mjini New York na California, Jenner alielezea kwa kina mapambano yake ya kuwa na jinsia mbili tangu utotoni.
''Akili zangu ni za kike sana kuliko za kiume.'' Ameongezea. '' Ni vigumu sana watu kuelewa, lakini hivyo ndivyo nafsi yangu ilivyo.''
Jenner aliyejawa na hisia na mwenye nywele ndefu shati na suruali ndefu alisema kuwa amesubiri kwa miaka mingi ili kujitangaza kwa kuwa hakutaka kuwavunja moyo watu.
Kwa miongo kadhaa wake wa zamani wa Jenner na madada zake waliweka siri kuhusu jinsia yake na kwamba walikuwa watu waliokuwa wakijua siri hiyo.
Mtandao wa watu wanaojua siri hiyo hatahivyo ulipanuka hivi majuzi wakati Jenner alipomwambia mamaake na wanawe 10 .
Jenner ana watoto sita Burt,Cassandra,Brabdon,Brody,Kendall na Kylie pamoja na watoto wanne wa kambo akiwemo Kourtney,Kim,Khloe na Rob Kardashian.

BBC

YANGA YATANGAZA UBINGWA RASMI BAADA YA KUWATANDIKA MAAFANDE WA POLISI MOROGORO

Yanga imefanikiwa kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya Vodacom kwa kuifunga Polisi Morogoro mabao 4-1 kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar, licha ya kuwa imesaliwa na mechi kadhaa kumaliza msimu wa 2014/2015. Wafungaji wa mabao ya Yanga leo ni Amiss Tambwe aliyefunga hat trick na Simon Msuva.

MASTAA WANAOONGOZA KUTUKANA\KUTUKANWA MTANDAONI

Tamrina Posh "Amanda" katika pozi

Imekuwa ikielezwa kuwa wasanii ni kioo cha jamii. Kwa maana hiyo wanatakiwa kufanya mambo ambayo yanaweza kuigwa na wale wanaowatazama. Hata hivyo, maisha wanayoishi baadhi ya wasanii hayaakisi msemo huo.
Wengi wamekuwa wakikumbwa na skendo mbalimbali zinazowafanya wasiwe na vigezo vya kuitwa kioo cha jamii.
Miongoni mwa mambo yanayowafanya wakati mwingine wadharaulike ni kutoa maneno machafu, ‘live’ au kupitia kwenye mitandao ya kijamii.

Katika makala haya nitawazungumzia mastaa wanaoongoza kwa kutukana mitandaoni lakini pia wale ambao wanaongoza kwa kutukanwa katika siku za hivi karibuni.

 Wastara Juma

Wastara…

Huyu Wastara amekuwa akiheshimika kwenye jamii kwa muda mrefu na alikuwa ni miongoni mwa mastaa wa kike ambao wangesimama na kuamua jambo wangesikilizwa kutokana na jinsi alivyokuwa amejiweka na kuwaaminisha watu.
Lakini katika siku za hivi karibuni alichafuka kwa kuingia katika orodha ya mastaa wanaotukana mtandaoni baada ya kumvaa mmoja wa mashabiki wake aliyemsemea mbovu na kumtukana matusi mazito
 “Iweje anakubali kushushwa na mtu mmoja ambaye alikaa na kuamua kumvuruga, anasahau kama kuna kundi la watu linamheshimu?”  Aliandika mmoja wa mashabiki wake kwenye mtandao wa Instagram baada ya kuona matusi hayo.

 Amanda Posh
Wafuatiliaji wa mambo na hasa wale ambao wapo Facebook watakumbuka jinsi staa huyu wa filamu alivyomshambulia jamaa mmoja aliyefahamika kwa jina la Joel.
Haikuwa ustaarabu kabisa kwa staa huyo kufanya hivyo kwani jambo lililomkasirisha angeweza kulipuuza na angebaki na heshima yake huku yule aliyemtukana akionekana mjinga.
Lakini ukiacha hilo, Amanda amekuwa akisifika kwa kutoa maneno machafu pale anapochokozwa, tabia inayomfanya afiti kwenye makala haya.


Isabela Mpanda
Katika mastaa micharuko, huyu yumo! Hajivuni, hajisikii lakini ukimchokoza lazima akushikishe adabu kwa matusi.
Posti zake zenye lugha chafu kwenye mtandao wa Instagram zipo nyingi lakini pia kwa wale wenye kumbukumbu watakumbuka kuwa staa huyu aliwahi kumtukana mwanamitindo Belina Mgeni na mpaka sasa hawaongei.
Hao ni baadhi ya mastaa ambao katika siku za hivi karibuni wameshika chati kwenye suala la kutukana mtandaoni.
Kwa upande wa wale ambao wanashika nafasi za juu kwa kutukanwa, wapo wengi lakini leo tutawazungumzia wahanga watatu.

 Kajala Masanja: 
Tangu aingie kwenye bifu na Wema Sepetu, kuna kundi ambalo linajiita Team Wema limekuwa likimshambulia kwa kumtukana na kumshutumu kwa mambo ambayo mengine hayana ukweli.
Hata hivyo, Kajala anaonekana kuwa mstaarabu kidogo kwani licha ya kutukanwa mtandaoni, yeye amekuwa mkimya akijua kujibizana na watu hao ambao wala hawana majina ni sawa na kuzidi kujichafulia.
Elizabeth Michael ‘Lulu’: Huyu naye ni mhanga wa matusi mtandaoni. Kuna kundi la watu ambao linaonekana kuwa na chuki dhidi yake, huenda kutokana na mafanikio aliyonayo akiwa kwenye umri mdogo.
 Lakini sasa, licha ya matusi anayoyaoga mtandaoni, amekuwa mvumilivu wa kuyaacha yapite. Watu wake wa karibu wanaeleza kuwa, licha ya kutukana sana mwenyewe wala hajui kwamba anatukanwa kwani si mtu wa kufuatilia nani kasema nini kibaya juu yake
Wema Sepetu:
Kama ilivyo kwa Kajala, huyu naye anashambuliwa sana na Team Kajala. Hawa ni watu ambao wamejitenga kuhakikisha wanamkosesha amani staa huyu.
 Amekuwa akitukanwa kwa mengi lakini kwa kuwa anajua ustaa ni kama jalala, huwa hajali na anachukulia poa.
 Ni mara chache sana amekuwa akinyanyua mdomo wake kuwajibu wale ambao wamekuwa wakimsema vibaya sambamba na kumtukana.
Kwa uchache hao ndiyo mastaa ambao hivi karibuni wametia fora kwa
 kutukana na kutukanwa mtandaoni.
Tahadhari
Mastaa ambao ni wepesi kutukana mtandaoni  wajue kwamba endapo Rais wa Jamhuri ya Muungano, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete atasaini ile sheria ya makosa ya mtandaoni ya mwaka 2015, watajikuta wanaenda jela hivi hivi.

GLOBAL PUBLISHERS








ZITTO KABWE NA WENZAKE WAZIDI KUPOTEANA..... CHAMA KINA WENYEVITI WAWILI.

Mwenyekiti wa ACT-Tanzania,  Lucas Kadawi Limbu (kulia) akisisitiza jambo.
 
 
MWENYEKITI wa Chama cha Alliance for Change and Transparency (ACT-Tanzania), Lucas Kadawi Limbu amemlalamkia Msajili wa Vyama vya Siasa Nchini, Jaji Mstaafu Francis Mtungi kwa madai ya kukiuka utaratibu wa kubadilisha jina la chama hicho na kuwa ACT-Wazalendo.
 
Limbu alitoa malalamiko hayo mbele za waandishi wa habari Dar es Salaam jana na kuhoji nyuma ya ACT-Wazalendo kuna nini.
 
"Tunashangazwa na jaji Mtungi kwa kubadili jina la chama chetu bila ya kufuata taratibu huku akijua fika kuna kesi ya msingi ipo mahakama kuhusu mwenendo wa chama hicho. Alisema Limbu

Aliongeza kuwa kuna njama za makusudi zilizofanywa za kubadilisha jina la chama hicho kwani haiwezeka na haiingii akilini kubadilisha jina la chama kwa kipindi kifupi na haraka kiasi hicho.

"ACT-Tanzania ni chama chetu sio cha Zitto na kama anahitahi siasa safi aanzishe chama chake kwani nafasi hiyo ipo wazi kwa kila mtanzania.

Alisema ni jambo la ajabu kuona chama kinafanya mkutano wake mkuu wenye nia hofu na kumpatia mtu madaraka ya kioongozi mkuu na kubadilisha jina lake huku msajili wa vyama akishuhudia.

Alisema msajili wa vyama vya siasa alitoa tamko la kubadilishwa jina la chama hicho tarehe 20-4-2015 wakati tayari kiongozi mkuu wa chama hicho kilichobadilishwa jina akiwa katika zaira ya kichama mikoani aliyoianza tarehe 10-4-2015 huku wakigawa kadi kwa kupitia chama cha ATC-Wazalendo.

Limbu alihoji fedha zinazotumika kwenye ziara hiyo na za kuchapa kadi, bendera za chama na vifaa vingine kuwa zinatoka wapi kama hakuna watu wenye nia mbaya na chama cha ATC-Tanzania.
(Imeandaliwa na mtandao wa http://www.habarizajamii.com/)

TASWIRA ZA ZARI NA DIAMOND WALIVYOJIACHIA VISIWANI ZANZIBAR

 Diamond akilibusu tumbo la mpenzi wake Zari ambaye ni mjamzito.…

 Mwanamuziki Nasibu Abdul 'Diamond' akijiachia na mpenzi wake Zarinah Hassan 'The Boss Lady' Visiwani Zanzibar.

Mwanamuziki Nasibu Abdul 'Diamond' akijiachia na mpenzi wake Zarinah Hassan 'The Boss Lady' Visiwani Zanzibar.


STAA wa Bongo Fleva nchini, Nasibu Abdul 'Diamond' na mpenzi wake Zarinah Hassan 'The Boss Lady' wamezidi kuonyesha kuwa penzi lao linazidi kuimarika baada ya Zari kuachia picha Instagram wakiwa 'close' walipokwenda Visiwani Zanzibar juzi.
Wapenzi hao walikuwa Zanzibar kwa ajili ya shoo ya Diamond iliyofanyika Jumamosi (Aprili 25, mwaka huu) usiku huko Ngome Kongwe.
Mojawapo ya picha za wapendanao hao imbayo imeenea mitandaoni ni ile ambayo Diamond analibusu tumbo la Zari mwenye ujauzito unaodaiwa kuwa wa staa huyo.

Global Publishers

MAKOMANDOO WA JWTZ WAPAGAWISHA SHEREHE ZA MUUNGANO

Makomandoo wakipita kwa ukakamavu mbele ya Rais Jakaya Kikwete wakati wa kuadhimisha miaka 51 ya Muungano kwenye Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam jana.


Dar es Salaam. Tanzania jana iliadhimisha miaka 51 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar huku viongozi wa upinzani wakisusia sherehe hizo za mwisho katika utawala wa Rais Jakaya Kikwete ambazo, makomandoo wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), walitia fora.
Rais Kikwete alikagua gwaride hilo katika sherehe zilizofanyika kwenye Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam na kuhudhuriwa na
viongozi mbalimbali pamoja na maelfu ya wananchi ambao baadhi walilazimika kutumia Uwanja Mkuu wa Taifa kufuatilia shughuli hizo.
Baadhi ya viongozi hao ni pamoja na, Makamu wa Rais, Dk Mohamed Gharib Bilal, Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein, Waziri Mkuu Mizengo Pinda, Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar, Maalim Seif Sharrif Hamad. Wengine ni Rais mstaafu, Benjamin Mkapa, Rais mstaafu wa awamu ya sita wa Zanzibar, Amani Abeid Karume na Waziri Mkuu Mstaafu, Frederick Sumaye.
Wapinzani wasusia
Viongozi wakuu wa vyama vya upinzani hawakushiriki maadhimisho hayo baadhi wakiwa mikoani katika shughuli za kuimarisha vyama vyao kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Oktoba.
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe yuko mkoani Kagera na Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba ambaye yuko mkoani Mtwara.
Hata hivyo, Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, James Mbatia, Kiongozi wa ACT – Wazalendo, Zitto Kabwe hawakuhudhuria na sababu za kutokuwapo kwao hazikuelezwa.
Wakuu waliokosekana
Pia, baadhi ya viongozi wa kitaifa hawakuonekana katika sherehe hizo akiwamo Rais mstaafu wa awamu ya pili, Ali Hassan Mwinyi, Mawaziri wakuu wa zamani, Jaji Joseph Sinde Warioba, John Malecela, Salim Ahmed Salim, Cleopa Msuya, Edward Lowassa.
Kikwete uwanjani
Kama ilivyo kawaida, msafara wa Rais Kikwete aliyekuwa na Mkuu wa Majeshi, Davis Mwamunyange katika gari maalumu la jeshi lililozungukwa na magari mengine saba na pikipiki 15, ulizunguka uwanja huku kiongozi huyo akipunga mkono na kushangiliwa kwa nguvu.

Hatua hiyo ilifuatiwa na wimbo wa Taifa sambamba na mizinga 21 na kisha Rais Kikwete ambaye pia ni Amiri Jeshi Mkuu alikagua gwaride la vikosi vya ulinzi na usalama.
Hata hivyo, wakati akikagua gwaride hilo, Rais Kikwete alipofika kwenye Kikosi cha Bendera, alisahau kupokea heshima hali iliyomfanya arudi nyuma kufanya hivyo kisha kuendelea kukagua vikosi vingine.
Baada ya hapo, ndege za kivita zilipita juu ya uwanja zikitokea Kaskazini kulekea Kusini mwa uwanja. Tukio hilo liliwafanya wananchi waliofurika katika uwanja huo kushangilia hasa kwa jinsi ndege hizo kivita zilivyokuwa zikifanya madoido angani.
Ndege hizo zilifuatiwa na gwaride la nje lililokuwa na vikosi 13 vikiongozwa na bendera ya Rais na ile ya JWTZ zilizokuwa sambamba na bendera saba, sita zikiwa ni za vikosi vya majeshi ya ulinzi na usalama pamoja na ya kikundi cha usindikizaji. Vilipita mbele ya Rais kwa mwendo wa haraka. Baadaye Vilifuata vikosi viwili; Kikosi Maalumu cha Wanamaji (Marine Special Force) na makomandoo vikiwa katika mwendo wa mchakamchaka.
Baada ya makomandoo kupita, alifuata askari polisi mmoja wa jeshi (MP) aliyepita peke yake kwa mwendo wa ‘digidigi’ na kushangiliwa kwa nguvu.
Makomandoo
Sherehe hizo zilikuwa na mvuto wa aina yake kutokana na manjonjo ya makomandoo hao walipokuwa wakipita mbele ya Rais Kikwete.
Kikosi cha makomandoo hao kikiwa katika mavazi ya kivita, bunduki, mabegi mgongoni hukuwa wakiwa wamepaka rangi nyuso zao, waliingia huku wakikimbia mchakamchaka na kushangiliwa kwa nguvu.
Halaiki
Sambamba na makomandoo, halaiki ya watoto iliyoonyesha mafunzo katika meli ya kivita nayo iliwanyanyua wananchi katika viti vyao kushangilia huku waliokaa jukwaa kuu wakiinua bendera na kuzipepea.
Halaiki hiyo iliyoingia uwanjani saa 5.10 ilianza kwa kutoa ujumbe wa sherehe hizo kwa mwaka huu ambao ni “Miaka 51 ya Muungano, Tudumishe Amani na Umoja, Ipigie Kura ya Ndiyo Katiba Inayopendekezwa na Kushiriki Uchaguzi Mkuu.” Kisha kuhamasisha kilimo wakisisitiza matumizi ya zana za kisasa. Pia, watoto hao wa halaiki walitoa ujumbe kupinga ujangili katika mbuga za wanyama ili kulinda maliasili hiyo kwa ajili ya vizazi vijavyo. Kadhalika, walihamasisha ujasiriamali wa kutumia kazi za mikono.
Kivutio kikubwa katika halaiki hiyo ilikuwa ni jinsi watoto hao walivyohamasisha ulinzi ambako walitoa ujumbe kuwa suala hilo ni jukumu la wananchi wote. Wakati wanatoa ujumbe huo walikuwa katika mwendo wa haraka huku wakienda mbele na nyuma na kutoa burudani nzuri kwa hadhira iliyokuwepo uwanjani hapo pamoja na watazamaji kupitia runinga.

Wakiendelea na onyesho la ulinzi, watoto hao walipita katika vikwazo huku wakiruka na kupita katikati ya maduara makubwa ya vyuma yaliyokuwa yanawaka moto na kisha kukanyaga makarai yaliyokuwa na moto pia.
Pia kulikuwa na watoto watatu waliopita juu ya kamba kwa staili tofauti na kuwavutia wazazi waliokuwapo. Wa kwanza alipita huku akining’inia kwa mikono yake. Alifuatiwa na aliyeshika kamba kwa mikono pamoja na miguu; uso ukielekezwa angani. Wa mwisho alipita juu ya kamba hiyo kwa kutambaa.
Mazoezi mengine ni yake ya mfano wa meli ya kivita yaliyokuwa yameandaliwa kwa umakini mkubwa. Watoto hao walipanda mnara wa meli hiyo kwa aina tofauti. Kuna aliyepanda kwa mikono pasipo miguu yake kugusa nguzo. Mwingine alipanda huku miguu yake ikiwa imenyooka mbele na wa mwisho alipanda kwa kuruka ruka.
Wakiwa bado ndani ya meli hiyo, mmoja alijifunga kamba mguuni na kuwanyanyua wenzake wawili kutoka chini. Ilikuwa ni mithili ya filamu nzuri ya kivita.
Kabla hawajaondoka, walipita katika mfumo wa vifaru vya kivita. Kimoja kikiwa cha kupiga masafa marefu na kingine mafupi. Watoto watatu walitengeneza matairi ya vifaru hivyo. Usingependa kuondoka wala kutaka watoto hao wamalize kuburudisha. Kwa hakika walivutia.
Ngoma, Kwaya
Baada ya halaiki zilifuata ngoma za makabila. Ngoma nne zilitumbuiza, mbili kutoka visiwani na nyingine bara. Pia kwaya kutoka Chunya, Mbeya ambayo ilifuatiwa na wimbo maalumu.
Wapongeza
Akizungumzia sherehe hizo, Spika wa zamani wa Bunge, Pius Msekwa alisema kudumu kwa Muungano ni suala la kujivunia kwani yapo mataifa mengine yaliyoshindwa.
“Tumepita katika mawimbi makubwa au kero za Muungano huu. Ingawa tumefanikiwa kuyavuka lakini ukweli ni kwamba yametuyumbisha sana. Ninaandika kitabu ambacho kinazungumzia historia ya Muungano tangu tulipouanzisha,” alisema Msekwa.
Alitoa mfano wa mataifa yaliyojaribu kuungana na kushindwa kuwa ni Senegal na Gambia; Malaysia na Singapore.
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere, Joseph Butiku alisisitiza vijana kujitokeza kwa wingi na kushiriki katika Uchaguzi Mkuu ujao.

Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Jaji Damian Lubuva alisema: “Nakumbuka sherehe za Muungano za mwaka 1977 niliteuliwa kuwa Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar na tangu hapo nimekuwa nikiitumikia Serikali. Ni siku ya kumbukumbu yangu muhimu katika maisha na taaluma pia,” alisema Jaji Lubuva.
Awali
Kabla ya sherehe hizo kuanza, milango ya Uwanja wa Uhuru ilifunguliwa saa 12.30 asubuhi na wananchi kutoka maeneo mbalimbali ya jiji kuanza kuingia. Mpaka inatimu saa 2.00 asubuhi uwanja huo ulikuwa umejaa na wananchi kulazimika kuingia Uwanja wa Taifa.

Ukawa waanza kugawana nchi, Wasambaa mikoani kutoa elimu.

Viongozi wa Ukawa

Dar/Mikoani. Katika kile kinachoonekana kuendelea kujiimarisha kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Oktoba, vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) vimegawana maeneo mbalimbali nchini vikifanya mikutano ya hadhara na mafunzo kwa viongozi wake ikiwa ni utekelezaji wa mkakati wa ushindi.
Ukawa unaundwa na vyama vya Chadema, NLD, NCCR-Mageuzi na CUF.
Chadema kilianza ziara zake mikoani wiki zilizopita baada ya kuzindua mkakati wake uitwao ‘Hakuna kulala, Hakuna kula, Mpaka Kieleweke’ nchi nzima wakati timu ya NCCR-Mageuzi ikiweka kambi mkoani Kigoma kwa kile ilichokiita kuimarisha majimbo ya kimkakati.
Sanjari na vyama hivyo, CUF tangu juzi kiliingia katika moja ya ngome zake, mkoani Mtwara pamoja na mipango mengine ya kiushindi, kinahamasisha wananchi kujitokeza kujiandikisha kupiga kura.
Jitihada za Ukawa kuzunguka mikoani zinakuja ikiwa ni majuma kadhaa tangu Chama cha Mapinduzi (CCM) kikiongozwa na Katibu Mkuu wake Abdulrahman Kinana kilipomaliza ziara ya kujiimarisha na kukagua utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya mwaka 2010.
Pia, ziara hizo ziligongana na zile za Chama cha ACT - Wazalendo zilizosababisha Chadema na chama hicho kipya kugongana Butiama.
ACT - Wazalendo kinachoongozwa na Zitto Kabwe kilihitimisha ziara yake ya kimkakati katika mikoa tisa inayoonekana kuwa ngome ya CCM, wiki iliyopita wilayani Bariadi, Shinyanga na kuvuna wanachama zaidi 6,000 katika mikoa hiyo.
NCCR-Mageuzi ipo Kigoma
Katibu Mkuu wa NCCR-Mageuzi, Mosena Nyambabe alisema jana kuwa Ukawa ina mikakati inayofanana ndani ya vyama vyao ya kuhakikisha inajiimarisha kisiasa nchi nzima ili ishinde Uchaguzi Mkuu.
Alisema siku 10 zilizopita, timu ya NCCR ikiongozwa na Makamu Mwenyekiti - Zanzibar, Haji Hamis Hamad ilianza ziara Kigoma kuhakikisha majimbo ya mkoa huo yanaendelea kuwa ngome yake.
“Kigoma nzima ina majimbo yetu ya kimkakati na Ukawa wameshatukabidhi sasa kilichobaki ni kufanya ‘political management’ (usimamizi wa kisiasa) katika kiwango kinachotakiwa.
“Katika kikosi hicho, pia wamo Katibu Mwenezi, David Kafulila, Katibu Mkuu Mstaafu, Samuel Ruhuza na Kamishna wa Kagera, Peterson Mshenyela na wengineo,” alisema Nyambabe.

Alisema baada ya kumalizika ziara katika mkoa huo viongozi hao wataelekea Kagera kwa kuanzia majimbo ya Ngara na Nkenge, maeneo ambayo Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe anaendelea kumwaga ‘cheche’.
Kinachoendelea katika ziara hizo ni kama mashambulizi ya ‘bandika bandua’ na kuzuia mparaganyiko ndani ya vyama hivyo ambao unaweza kutokea baada ya kuanza kwa mchakato wa kugawana nafasi za udiwani na ubunge.
Chadema kila kona
Chadema, inayoendelea na utoaji wa mafunzo ya uongozi bora kwa viongozi wa ngazi zote na makada waliotia nia ya kugombea na mikakati mingine ya ushindi, viongozi wake wa juu wametawanyika maeneo tafauti katika kanda zake 10 za kiutendaji.
Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willbrod Slaa aliyekuwa Morogoro alieleza kuwa Tanzania kwa sasa inasifika nje ya nchi kwa uvunjifu wa haki za binadamu.
Akizungumza wakati wa mkutano wa hadhara kwenye Uwanja wa Shule ya Msingi Kiwanja cha Ndege, Manispaa ya Morogoro juzi, Dk Slaa alisema katika kipindi cha miaka mitano, utawala wa Rais Jakaya Kikwete umekuwa na matukio mengi ya uvunjaji wa haki za binadamu.
Alisema hivi karibuni alikuwa Marekani kwa ziara maalumu na huko alihojiwa na waandishi wa habari katika kituo kimoja cha redio juu ya masuala ya utawala bora nchini.
Naibu Katibu Mkuu wa Chadema (Zanzibar), Salum Mwalimu akiwa mkoani Rukwa alisema CCM imepoteza baraka za Mungu kiasi cha kushindwa kujua mgombea wake wa urais mpaka sasa, jambo ambalo halijawahi kutokea katika historia ya chama hicho.
Mwalimu aliyekuwa akizungumza kwenye Ukumbi wa Libori Mjini Sumbawanga, alisema viongozi wanaotokana na Chadema wapaswa kuwa tayari kusimamia haki kwa gharama zozote, kukataa rushwa na kupunguza kero kwa wananchi na kuwaonya wasije wakaufanya utawala wa Chadema kuwa kama wa CCM ambayo inayumba.
“Tuna miezi mitatu imesalia tuanze kampeni, lakini mpaka sasa CCM haijamjua mgombea wake, lini imewahi kutokea? Mungu amewachanganya kama wajenzi wa karavati,” alisema Mwalimu ambaye baada ya mkutano huo aliendelea na ziara yake mjini Makambako, Njombe.
Mwalimu alionyesha kushangazwa na baadhi ya wafuasi wa Chadema kujiunga na chama cha ACT – Wazalendo na akakiita kuwa ni chama cha msimu ambacho kitapotea baada ya Uchaguzi Mkuu.
Akiendelea na ziara yake mkoani Kagera, Mbowe alisema kusuasua kwa uandikishaji wa wapigakura ni kiashiria cha uvunjifu wa amani inayotokana na hofu ya CCM kuangushwa Oktoba.

Akiwahutubia wakazi wa Mji wa Bukoba juzi katika Uwanja wa Uhuru, Mbowe alisema nchi inaweza kuingia katika machafuko endapo litakuwapo jaribio lolote la kuahirisha Uchaguzi Mkuu kama upigaji kura wa Katiba Inayopendekezwa ulivyoahirishwa.
Alisema uchaguzi siyo suala la dharura na kila hatua inatakiwa kuwekwa wazi ili kuondoa hofu iliyoanza kujengeka kutokana na kubakia miezi michache kabla ya Uchaguzi Mkuu.
Profesa Lipumba, Mtwara
Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba amesema kuwa endapo Wapinzani wataingia madarakani, kazi ya kwanza itakayofanyika ni kufumua mikataba yote iliyoingiwa bila kufuata taratibu.
Alisema asilimia kubwa ya mikataba iliyoingiwa na Serikali, haiwanufaishi Watanzania walio wengi na zaidi ya hapo haina tija kwa Taifa.
“Haiwezekani Watanzania wakaishi katika hali ya umaskini wakati wana rasilimali nzuri, zinazowafanya wafaidi matunda ya nchi yao, lakini kuna wajanja wachache wanaingia mikataba isiyo na tija, sasa tukiingia madarakani, tutaifumua,” alisema Profesa Lipumba ambaye leo atakuwa Kijiji cha Msimbati.
Juzi, akiwa katika Mji wa Mikindani mkoani Mtwara aliionya Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kuacha kushughulikia suala la Kura ya Maoni ya Katiba Inayopendekezwa na badala yake ijikite kuandaa mazingira ya kufanyika kwa Uchaguzi Mkuu ili kulinusuru Taifa kuingia katika mgogoro usio wa lazima.
Profesa Lipumba alisema NEC isipoteze rasilimali za Taifa na muda kwa jambo lisilo na tija kwa wakati huu.
“Jaji Lubuva (Damian, Mwenyekiti wa NEC) asiliingize Taifa katika mgogoro, ana haraka gani na Katiba Inayopendekezwa wakati hili la uandikishaji katika Daftari la Kudumu la Wapigakura hajalimaliza...? Ashughulikie hili la daftari ndiyo kazi yake kwa sasa, siyo Katiba,” alisema Profesa Lipumba huku akishangiliwa na wananchi.

Credit: Mwananchi

Saturday, April 25, 2015

Chadema yaifanyia umafia CCM

Ukerewe. Chama cha Demokrasia na Maendeleo(Chadema) kimeweka mkakati utakaowafanya makada wake wavamie majimbo yanayoshikiliwa mapema na CCM, huku wakichelea kuingia kwenye majimbo yaliyo chini ya chama hicho kikuu cha upinzani.
Mkakati huo ulitangazwa jana na Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe wakati akihutubia mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye Uwanja wa Mongella mjini hapa, mkutano ambao ulifurika maelfu ya watu.
Mbowe alitangaza kupiga marufuku wanachama wa Chadema kuanza kutangaza nia kwenye majimbo ambayo wenzao wanayashikilia hadi hapo Bunge la Jamhuri ya Muungano litakapovunjwa.
Lakini alisema wanachama wa Chadema wanaruhusiwa kuanza purukushani kwenye majimbo ambayo yanashikilia na vyama vingine hasa chama tawala cha CCM ambacho kinashikilia majimbo mengi.
“Naomba ifahamike Chadema ni zaidi ya ubunge, tunahitaji amani na siyo kuharibu chama. Chadema itasimamisha watu makini kwenye maeneo yote katika uchaguzi huu,” alisema mwenyekiti huyo ambaye yuko kwenye ziara ya mikoa ya Kanda ya Ziwa.
Mbowe ambaye hakugusia suala la Ukawa katika mkutano huo, alisema kuwa utaratibu utaandaliwa wa kupata wagombea na kwamba hata waliokuwa wabunge, wasijihakikishie kuwa watapitishwa tena kwenye maeneo yao wanayoyaongoza sasa.
“Tutakuja na utaratibu mwingine. Hata wabunge wa Chadema waliokuwa katika maeneo hayo, wasidhani kwamba watabakia hapo. Tutasimamisha mtu anayekubalika na watu wote, na utaratibu ukiwekwa, hata aliyekuwa mbunge anaweza kuondolewa,” alisema Mbowe.
Alisema kuwa Chadema inaamini kuwa katika kila eneo kuna mtu wake ambaye ni makini na ni wazi atashinda.
Vyama vinne vya upinzani, Chadema, NLD, NCCR-Mageuzi na CUF vimekubaliana kusimamisha mgombea mmoja kuanzia kwenye uchaguzi wa madiwani hadi rais. Vyama hivyo, vilivyo chini ya mwavuli wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), vimekubaliana kuwa kila chama kipate mgombea wake na baadaye vitachambua anayekubalika na wengi.
Ainanga Nec
Akizungumzia mwenendo wa uboreshaji wa Daftari la Wapigakura, Mbowe alisema Taifa kwa sasa liko kwenye giza nene kutokana na maandalizi mabovu ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi(Nec).
Mbowe alisema kucheleweshwa kwa kazi ya uandikishaji wapigakura ni sehemu ya njama za CCM kupitia Serikali yake inayotamani kutumia nafasi hiyo ili kuendelea na hujuma katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba.

NYALANDU‏: TEMBO KUTOWEKA TANZANIA MIAKA 10 IJAYO

Waziri wa Maliasili na Utalii, Mh. Lazaro Nyalandu akizungumza katika mkutano uliohusisha wadau wa mashirika ya Kimataifa na asasi za kijamii ukiwa na lengo la ushirikishaji wa jamii katika masuala ya uhifadhi wa wanyamapori uliofanyika jana katika ukumbi wa mikutano wa Mpingo House uliopo Wizara ya Maliasili na Utalii jijini Dar es Salaam. 
 Waziri Nyalandu akiendelea kutoa ufafanuzi.
 Waziri Nyalandu akikazia jambo.
 Naibu Waziri wa Maliaisli na Utalii, Mahmoud Mgimwa akitoa salamu kwa wadau wa taasisi za kirai. Kushoto Waziri wa Maliasili na Utalii, Mh. Lazaro Nyalandu.

Mratibu wa Uhakiki wa Ubora kutoka Haki Elimu, Robert Mihayo akitoa maoni kwa Waziri Mh. Nyalandu ambapo amemuomba kushirikisha wadau wa elimu katika kutoa elimu ya uhifadhi wa wanyamapori kuanzia ngazi ya elimu ya msingi ili kuwaanda vijana ambao ni taifa la kesho.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Foundation for Civil Society, Francis Kiwanga akishiriki kutoa maoni katika masuala ya uhifadhi wa wanyamapori pamoja na kutokemeza ujangili wa Tembo.


WAZIRI wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu amesema kama watanzania wasiposhirikiana katika kudhibiti ujangili wa Tembo waliopo watatoweka kabisa katika kipindi cha miaka 10 ijayo.
Kauli hiyo ameitoa jana kwenye mkutano wa ushirikishwaji wa jamii katika masuala ya uhifadhi wa wanyamapori uliofanyika wizarani kwake.
“Uhifadhi kama tunavyoujua, hautaweza kufanikiwa kama kila mtu kwenye nchi hii atafikiria ni kazi ya serikali kuu peke yake.
Na vilevile kama kila mtu atafikiria ni kazi ya wahifadhi peke yao”. alisema Nyalandu kwenye mkutano huo.
Nyalandu alibainisha kuwa, majadiliano hayo, yatakuwa chachu kubwa ya maendeleo katika wizara hiyo huku akiwashukuru wadau hao mbalimbali wakiwemo wanahabari kwa kufika kwao, ili kuangalia suala la uhifadhi kwa mapana yake.
Alisema wakati ujangili wa Tembo nchini umeshamiri sana, wakati umefika kwa watanzania kuhakikisha kwamba wanakomesha hali hiyo ili taifa kuendelea kuwa na wanyama wake.
Alisema mathalani Tembo katika hifadhi ya Selous wamepungua kutoka Tembo 38,975 katika sensa ya mwaka 2009 hadi Tembo 1,384 kwa sensa ya mwaka 2014 na akasema kwa kasi hiyo katika miaka 10 ijayo Tembo Tanzania wataisha kabisa.
“Hili ni muhimu watu wakafahamu, upana wa hivi vita ni mkubwa kiasi gani na watu wanaohusika ni wengi kiasi gani ndani na nje ya nchi," alisema Nyalandu akiongeza kuwa mitandao ya kihalifu imetanda ulimwenguni kote.
Alisema suala la hifadhi halipo kwa wanyama pekee bali lipo katika upana wote na hata katika misitu.
Alisema ili kukabiliana na ukatwaji hovyo wa miti kutoka katika misitu ya miombo wanajipanga kuhakikisha kwamba miombo inayodaiwa kuingizwa nchini kutoka Zambia inakamatwa ili kulinda miombo iliyopo magharibi ya nchi.
Akizungumzia suala la mifugo na mbuga zinazopakana nazo amesema kwamba wanaanda rasimu ya kuhakikisha kwamba kuna mahusiano mazuri kati ya wenye mifugo na hifadhi wakiwa tayari kuyaachia baadhi ya maeneo kwa lengo la kuhakikisha kwamba wafugaji hawaingizi mifugo yao katika hifadhi.
Aidha amesema kwamba wanajipanga namna ya kuhakikisha kwamba hakuna mgongano wa maeneo kati ya wanyama na binadamu na kwamba wanavijiji wanafundishwa namna ya kuishi na wanyama katika maeneo yenye mwingiliano mkubwa.
Aidha alisema kwamba meno ya Tembo kilo 1,763 yalikamatwa mwaka jana na jitihada zinaendelea za kukabiliana na majangili kwa kutanua mtandao wa kiintelejensia ndani na nje.
Alisema kwa sasa wanamsaka raia wa China anayeshutumiwa kutorosha nyara za serikali kwa kushirikiana na jeshi la Polisi la Kimataifa (Interpol).
Kwa nje ya nchi, meno ya Tembo yaliyokamatwa, Kilo 40 katika miji ya Hong Kong, China.
Aidha alisema watuhumiwa 1,711, walikamatwa kuanzia Januari hadi Desemba mwaka jana na kesi zao zinaendelea katika mahakama mbalimbali hapa nchini. Pia silaha 85 zimekamatwa ikiwemo silaha za kivita ambazo walikuwa wakizitumia mbugani.
Alisema ukichanganya na silaha zilizokamatwa kwenye operesheni tokomeza, jumla silaha 1,199 zimekamatwa.
Kwa upande wake, Ali Said Mosee aliyehudhuria mkutano huo kutoka Tanzania Association on Climate Change, alishauri ushirikishaji wa wadau mbalimbali kutatua migogoro kwenye mipaka ya mbuga na pia mgongano wa kimaslahi kati ya hifadhi na wanadamu.
Aidha wadau walishauri Wizara kuhakikisha inapunguza misafara ya wanyama ya kuhamahama kutoka sehemu moja hadi nyingine ikiwemo kwa kuzalisha miti na mazao yanayopendwa na wanyama hao.
“Wanyama wetu wanatakiwa wafanyiwe utafiti na kujua nini Nyati anapendelea kula porini, basi wapande hiyo miti na vyakula vyake kwa ujumla hata kwa Tembo hivyo hivyo.Wapande hiyo miti hapa hapa kwani hata siye binadamu tunavyovyakula tunavyovipenda, naamini hata kwa wanyama ni hivyo hivyo, rai yangu ni kuwa tufanye utafiti na kujua ili kuzuia misafara hii” alisema Ali Said Mosee.
Tanzania inahifadhi za taifa 16 na asilimia 40 ya ardhi ya nchi ni maeneo yaliyohifadhiwa. Kati ya maeneo hayo yaliyohifadhiwa hadi mwezi uliopita mwaka huu 2015, maeneo 19 yanamilikiwa na wananchi na yameshasajiliwa. Pia alisema kwamba kuna mapori ya akiba, 28 nchi nzima.
“Watu wengi wanadhani kwamba misitu yote inamilikiwa na serikali kuu. Ukweli ni kwamba serikali kuu inamiliki asilimia 35 tu ya misitu ya nchi yetu, misitu mingine yote inamilikiwa na vijiji, wilaya na watu binafsi asilimia 7. " alibainisha waziri huyo.
Aliwataka watendaji wa Serikali za mitaa kukabiliana na changamoto ya kutoweka kwa kasi kwa misitu ili taifa lisitumbukie katika jangwa.