Sunday, June 15, 2014

MAKUNDI YA URAIS YAZIDI KUIVURUGA UVCCM, MOROGORO WAMKATAA MWENYEKITI WAO....




Baadhi ya wajumbe wa UVCCM kutoka wilaya mbalimbali za mkoa wa Morogoro wakiwa na mabango ya kumkataa Mwenyekiti wa UVCCM mkoa wa Morogoro Herieth Sutta anayedaiwa kushindwa kuongoza.

 Wajumbe wa UVCCM wakiingia ukumbi wa hoteli ya Usambara kwa mabango na nyimbo za kumkataa mwenyekiti wao kabla ya kikao chao cha  Baraza la Vijana Mkoa wa Morogoro.

 Mwenyekiti wa UVCCM mkoa wa Morogoro Herieth Sutta anayelalamikiwa na wanachama wake akidaiwa kushindwa kuwaongoza.

 Herieth Sutta (kulia) akiwa na Kamanda Mkuu wa UVCCM Taifa, Mzee Kingunge Ngombale Mwiru ambaye alikuwa mgeni rasmi katika kikao hicho cha Baraza la Vijana Mkoa wa Morogoro.

 Kamanda wa UVCCM Taifa, Mzee Kingunge Ngombale Mwiru (kushoto) akimsimika Kamanda wa UVCCM Wilaya ya Morogoro Mjini, Pascal Kihanga ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama Cha Soka Mkoa wa Morogoro (MRFA).

GPL

No comments:

Post a Comment