Monday, June 16, 2014

MAIMARTHA AHUSISHWA NA KASHA YA UTAPELI... MWENYEWE AKATAA KATA KATA

SKANDALI! Prizenta maarufu Bongo, Maimatha Jesse amejikuta katika wakati mgumu baada ya kukwaa skendo ya utapeli kutokana na dawa za kukuza maungo anazoziuza kuwa hazifanyi kazi.
Sosi ameibua utapeli huo wa Maimatha kwa kusema:

 Prizenta maarufu Bongo, Maimatha Jesse akipozi katika duka lake la vipodozi.

 “Maimatha anatapeli watu na dawa zake, yaani tumepaka mabinti wengi hazitusaidii chochote, ni wizi mtupu, laki mbili bila chochote kweli roho inauma.”

 Maimatha Jesse.

Baada ya kunyaka madai hayo, Ijumaa Wikienda lilimtafuta Maimatha akakanusha:
“Hao wamejisikia tu kuongea hata siwafahamu na wala sijawahi kupata kesi kama hizo, mbona nilishawauzia wengi? Mimi mwenyewe zimenisaidia, wazushi tu,” alisema Maimatha.

No comments:

Post a Comment