Friday, May 16, 2014

TAZAMA JINSI MHESHIMIWA EDWARD LOWASSA ANAVYOKANUSHA KUHUSIKA NA KUNDI LA MATAPELI WA FOCUS VICOBA

Waziri Mkuu aliyejiuzulu na Mbunge wa Monduli Mh. Edward Ngoyai Lowassa


Napenda kutoa taarifa rasmi kuwa watu wasiojulikana na wenye nia ovu na mimi Edward Ngoyai Lowassa wamekuwa wakiweka taarifa kwenye mitandao ya kijamii kwa lengo la kunichafua mimi na pia kufanya utapeli kwa nia mbaya.ya kutumia jina langu..
Jina langu limetumiwa kutoa habari za uongo.katika ukurasa wake wa Facebook mtu anayejiita Francis Heri Hoza ameandika habari ya kwamba Mh Lowassa ametoa kiasi cha shilingi millioni 300 kwa mfuko wa vicoba uitwao Focus Vicoba.
Na pia ameandika kuwa Mh Lowassa ametamka hayo katika mahojiano na Kituo cha Radio Cha East Africa.Chanzo cha habari yake hiyo ni akaunti ya twitter yenye jina la Mh Lowassa.
Ofisi ya Mh Lowassa inachukua nafasi hii kukanusha kwa nguvu taarifa hiyo iliyojaa uongo. na pia akaunti ya twitter iliyotumika kama chanzo cha habari hiyo,haihusiani kwa namna yoyote na Mh Lowassa.
Nawasihi watanzania na nasisitiza tena kwa wananchi wenzangu kutumia mitandao ya kijamii kwa manufaa na maendeleo na siyo kutoa habari za kupotosha jamii.
AC RASMI YA Edward Ngoyai Lowassa YA TWITER NA FACEBOOK NA TOVUTII NI HII HAPA.M http://www.elowassa.com/index.php
Imetolewa na ofisi ya Mh Edward Lowassa(MB)

No comments:

Post a Comment