Tuesday, June 24, 2014

PENZI LA MTUNISI NA BATULI LAFUFUKA UPYAAA....TAZAMA HAPA

WASANII wawili wa filamu, Nice Mohamed ‘Mtunisi’ na Yobnesh Yusuph ‘Batuli’ ambao walikuwa wapenzi kabla ya kuachana na mwanaume huyo kuoa, sasa wamerudiana rasmi.

 Staa wa filamu Bongo Yobnesh Yusuph ‘Batuli’.

 Kwa mujibu wa chanzo chetu kilicho jirani na wasanii hao kimesema wawili hao hivi sasa wanapika na kupakua.Kilisema baada ya kurudiana, kwa sasa wanaishi pamoja kama mume na mke maeneo ya Sinza, jijini Dar es Salaam huku wakiishi kwa amani na upendo.
“Yaani sasa hivi Batuli na Mtunisi wana mahaba niue kwani wanaishi pamoja wanaamka na kulala wote maeneo ya Sinza-Mawela lakini wanafanya kuwa ni siri yao, hawataki watu wajue,”kilisema chanzo hicho.
Hivi karibuni Batuli aliweka picha ya Mtunisi katika akaunti yake kwenye mtandao wa Instagram na kuandika maneno haya “Alichokipanga Mungu hakuna wa kukipangua.”

 Nice Mohamed ‘Mtunisi’.

Alipotakiwa kuzungumzia suala hilo, Batuli alisema hawezi kuzungumzia katika vyombo vya habari kwa vile mambo hayo ni maisha yake binafsi.
Kwa upande wake, Mtunisi alicheka na kudai kusikia kutoka kwa watu juu ya mwenzake kuweka picha yake mtandaoni na kuandika maneno ya kimahaba, kitu alichosema hawezi kuzuia nafsi ya mtu kumuweka moyoni.

No comments:

Post a Comment