Tuesday, June 10, 2014

KUELEKEA 2015: MTOTO WA KAPTENI KOMBA AJIUNGA NA CHADEMA..... AIPONDA CCM

Gerald John Komba,jana aliamua kuvua gamba na kubwaga manyanga ya CCM na kujiunga na CHADEMA

 Miezi kadhaa tangu mbunge wa Mbinga kwa tiketi ya CCM kapten John Komba autangazie umma kwamba ataingia msituni kuanzisha vita iwapo mfumo wa serikali 3 utapita,mtoto wake aitwaye Gerald John Komba,jana aliamua kuvua gamba na kubwaga manyanga ya CCM na kujiunga na CHADEMA,bwana Komba ambaye amehitimu shahada yake ya sheria chuo cha SAUT mwaka jana alikuwa chuoni hapo kuchukua vyeti vyake vya elimu,ndipo alipoamua kujiunga na CHADEMA tawi la SAUT,akizungumza na mwandishi wa habari hii juu ya sababu zilizompelekea yeye kuamua kuachana na chama cha babayake alisema
"Unajua ndugu yangu Kilunga,ukiwa chuo huwezi ukayaona maisha halisi ya mtaani,mtaani ndo field kamili na ngumu,lakini ukiwa chuo tena ukiwa mtoto wa kigogo huwezi ona umuhimu wa kuvisapoti vyama vya upinzani,binafsi nimeenda nyumbani Mbinga na sehemu kadhaa za nchi wananchi wanateseka sana,"alimaliza kuongea kijana huyo ambaye pia anakipaji cha uimbaji kama babayake,alipoulizwa na mwandishi wa habari hii kama anampango wa kwenda kumng'oa baba yake jimboni Mbinga kupitia CDM alisema hilo lingewezekana akiwa CCM bt kwa CDM hafikirii kama hilo linawezekana kwani CHADEMA hakuna sera za kurithishana majimbo ama uongozi kama ilivyo kule CCM huku akitolea mfano wa majimbo ya Chalinze na Kalenga,alipotakiwa azitolee ufafanuzi wa picha kadhaa zilizorushwa mitandaoni zikimwonesha baba yake akiwa katika mikao tofauti ya kimapenzi na binti mmoja alisema"japo katika siasa lolote linawezekana bt kwa hili la picha nipo pamoja na mzee,picha zile hazina uhalisia bali ni za kutengenezwa ili kumchafua mzee"


 Haya yanatokea wakati ambao katibu wa itikadi na uenezi CCM Nape Moses Nnauye,akiutangazia umma kwamba ameisambaratisha CDM chuoni SAUT kufuatia ziara yake iliyofanyika siku 2 zilizopita na kufanikiwa kuwachukua wanachama wawili waliokuwa tayari wamefukuzwa CDM SAUT kwa tuhuma mbalimbali ikiwemo za usaliti na kuhongwa pesa ili walivuruge tawi hilo la CHADEMA chuoni hapo.
Picha chini aliyevaa shati la mistari ni Gerald Komba alipokuwa akikabidhiwa kadi na katibu mwenezi wa tawi la SAUT ndugu Jovinary Benson tawini hapo.

1 comment:

  1. kweli hakuna mtu mwembembe,, hadi huyu jamaa kanenepa.. kweli ameanza kuwa mkubwa,, tangu enzi za mbezibeach high

    ReplyDelete