Tuesday, June 24, 2014

ALSHABAAB WAFANYA UNYAMA MWINGINE KENYA, WAUA WATANO

Mabaki ya magari katika shambulio la Mpeketoni.

WATU watano wamepoteza maisha baada ya shambulio lililotokea usiku wa kuamkia leo katika kijiji cha Pandanguo huko Witu wilayani Lamu nchini Kenya kilometa 30 kutoka Mpeketoni yalipotokea mauaji ya watu zaidi ya 60 wiki iliyopita.
Polisi wamesema kuwa waliouawa ni kutoka jamii mbalimbali.
Mkuu wa Polisi nchini Kenya, David Kimaiyo amesema kuwa washambuliaji walivamia kijiji cha Pandanguo na kuua takribani watu watano.
"Bado tunawasaka waliohusika na shambulio hili, habari zaidi zitatolewa baadaye," alisema Kimaiyo.

No comments:

Post a Comment