Tuesday, May 6, 2014

HATIMAYE RIDHIWANI KIKWETE NA GODFREY MGIMWA WAAPISHWA RASMI LEO BUNGENI.

Hatimaye wabunge wapya wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ridhiwani Jakaya Kikwete ambaye amechaguliwa hivi karibuni kuwa mbunge wa Jimbo la Chalinze baada ya kifo cha aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo Saidi Bwanamdogo, na kijana Godfrey Mgimwa ambaye amechaguliwa kuwa mbunge wa jimbo la Kalenga kufuatia kifo cha aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo William Mgimwa ambaye ni baba yake.


                 Wakati wa kufungua kikao cha Bunge la bajeti kwa mwaka 2014, Dodoma leo asubuhi.



                    Familia za waheshimiwa wabunge wapya Ridhiwani Kikwete na Godfrey Mgimwa wakifuatilia kwa makini tukio la kuapishwa wabunge hao vijana, leo asubuhi.





Mama Salma Kikwete na Mama Mgimwa wakiteta jambo, Bungeni leo asubuhi.


Godfrey Mgimwa akila kiapo cha kulitumikia jimbo la Kalenga kama mbunge wake leo asubuhi.

Mbunge mpya wa jimbo la Chalinze, Ridhiwani Kikwete akiapishwa leo Bungeni.

No comments:

Post a Comment